Wednesday 8 August 2018

Mkalama yang'ara Nanenane Kanda ya kati

Naibu Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Anthony Mavunde (kulia) akimkabidhi cheti cha Ushindi Afisa Mifugo wa Wilaya ya Mkalama Bw. Elias Mbwambo baada ya Wilaya hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa halmashauri za wilaya zilizopo Mkoani Singida kwenye kilele cha maadhimisho ya 22 ya Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji (NANENANE)  Nzuguni jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Daktari Rehema Nchimbi akimpongeza Afisa Mifugo wa Wilaya ya Mkalama Bw. Elias Mbwambo baada ya Wilaya hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa halmashauri za wilaya zilizopo Mkoani Singida kwenye kilele cha maadhimisho ya 22 ya Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji (NANENANE) hapa Nzuguni jijini Dodoma.

Wawakilishi wa wakulima wa Wilaya ya Mkalama wakijumuika na viongozi wa Idara za Kilimo na Mifugo za Wilaya hiyo kufurahia ushindi baada ya Wilaya hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa halmashauri za wilaya zilizopo Mkoani Singida kwenye kilele cha maadhimisho ya 22 ya Sikukuu ya Wakulima na Wafugaji (NANENANE) Nzuguni jijini Dodoma.




“RUDI MKALAMA, KUMENOGA!”   Hiyo ndio kauli inayoweza kutumika hivi sasa baada ya Wilaya ya Mkalama kufanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwa Halmashauri za Mkoa wa Singida kwenye maonesho ya 22 ya sikukuu ya wakulima na Wafugaji (NANENANE)  yaliyohitimishwa leo hii na Naibu Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Anthony Mavunde.

Ushindi huo  unatokana na Wilaya hiyo kujidhatiti kikamilifu katika sekta za Kilimo na Mifugo ambapo waliweza kuonesha kwa vitendo kwa kuotesha mimea mbalimbali inayolimwa Wilayani Mkalama kupitia mashamba yao yaliyopo hapa kwenye viwanja vya Nzuguni.

Mbali na mimea hiyo iliyostawi vizuri, Mkalama pia wameweza kuonesha ustadi wa kufuga samaki na kuku ambapo wataalam wa mifugo na uvuvi waliweza kuonesha namna bora kabisa ya kufuga kuku wa kienyeji na aina mbalimbali za samaki kupitia bwawa lililopo nyuma ya banda lao  la Maonesho.

Katika hali inayoonesha kujipanga zaidi kwa Uongozi wa Wilaya ya Mkalama katika maonesho yajayo, Wilaya hiyo imeshatengeneza mabanda ya kufugia Ng’ombe na Mbuzi hivyo kwa wageni watakaotembelea banda hilo kwenye maonesho ya mwaka 2019  watapata fursa ya kujifunza namna bora ya kufuga ng’ombe na mbuzi.

Mkalama Guntooooooo!



No comments:

Post a Comment

HALMASHAURI YA WILAYA MKALAMA