Wednesday 2 August 2017

Hongereni Mkalama- Nchimbi




Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe: Daktari Rehema Nchimbi akizungumza na Baraza la madiwani na wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wakati wa kujadili hoja mbalimbali za ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) mapema jana.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Bi. Anjelina Lutambi akizungumza kwenye  Baraza la madiwani na wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wakati wa kujadili hoja mbalimbali za ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) mapema jana.



Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhe: James Mkwega akizungumza kwenye  Baraza la madiwani na wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wakati wa kujadili hoja mbalimbali za ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) mapema jana.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Godfrey Sanga akizungumza kwenye  Baraza la madiwani na wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wakati wa kujadili hoja mbalimbali za ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) mapema jana.


Pongezi kubwa zimetolewa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kufuatia kupata hati safi kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe: Rehema Nchimbi wakati wa kikao cha kujadili hoja mbalimbali zilizoainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali kilichojumuisha Mkuu wa Wilaya hiyo, madiwani wote wa Halmashauri ya Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri na Wataalam wa idara mbalimbali katika Wilaya hiyo.

“Sina wasiwasi na Wilaya ya Mkalama kwa sababu inaongozwa na Wahandisi katika nafasi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya na ndio maana kazi zote zilizofanyika katika Wilaya hii zimefanyika kitaalam” Alisema Mhe: Nchimbi.

Mhe: Nchimbi alisema kuwa jambo hilo limeifanya halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kuwa na sifa ya kipekee ukilinganisha na Wilaya nyingine kwa sababu changamoto inayoyakabili maeneo mengi ni ukosefu wa wahandisi hali inayosababisha kila mradi kutotekelezwa kitaalam.

“BOQ ya mwanzo ya jengo hili haikuwa na sura nzuri lakini Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya waliweka taaluma zao hapa tena bila kulipwa na kutengeneza BOQ ambayo imelifanya jengo hili kuwa la mfano katika Ofisi zilizojengwa kwa fedha ya serikali” Aliongezea Mhe: Nchimbi.

Katika hatua nyingine Mhe: Nchimbi ameagiza kukarabatiwa kwa boma la Mkalama lililokuwa likitumiwa na Serikali ya Ujerumani wakati wa Ukoloni na hatimaye liweze kutumika kama chanzo cha mapato ya Halmashauri.

“ Naomba Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na Wataalam wako mkishirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na wadau mbalimbali  mkae chini na mniletee andiko litakaloonesha ni jinsi gani mnaweza kulifanya boma hili kuwa chanzo cha mapato ya Halmashauri ya Wilaya na andiko hilo nilipate  Agosti 28 mwaka huu” Alimalizia Mhe: Nchimbi.

Kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida bonyeza hapa.


No comments:

Post a Comment

HALMASHAURI YA WILAYA MKALAMA