Hizi ndio pikipiki walizokabidhiwa maafisa elimu kata leo. |
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka amekabidhi jumla ya pikipiki 17 zilizotolewana shirika lilisilo la kiserikali linalojulikana kama “EQUIP-T” ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na shirika hilo kama sehemu ya kuwapa hamasa maafisa elimu kata wilayani hapa.
Hafla hiyo fupi ilifanyika mapema leo asubuhi kwenye
viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambapo Mhe. Masaka
aliwataka maafisa elimu hao kuhakikisha wanatumia vyombo hivyo vya usafiri
kuinua kiwango cha elimu wilayani Mkalama.
“Pikipiki hizi sio za matumizi binafsi na msizitumie
kwenda kwenye michepuko yenu kwa sababu tunahitaji kuona pikipiki hizi
zinapunguza idadi ya mimba shuleni na zinaongeza kiwango cha ufaulu”
Alisisitiza Mhe. Masaka.
Kwa upande wake mwakilishi wa maafisa elimu kata hao ambaye pia ni Afisa elimu kata
wa kata ya Msingi, Bw. Elisante Mbazi aliishukuru serikali na shirika la
EQUIP-T kwa vitendea kazi hivyo ambapo kwa niaba ya maafisa elimu kata wenzake,
aliahidi kutumia pikipiki hizo kuongeza kiwango cha ufaulu na kuboresha elimu
kwa ujumla wilayani Mkalama.
“Tulikuwa tunapata changamoto ya kuzifikia baadhi ya shule
kwa ajili ya ufuatiliaji lakini sasa kupitia pikipiki hizi za kisasa,
changamoto hiyo imeisha” Alimalizia Mbazi.
Pikipiki hizo zilizokabidhiwa leo zilikuwa na
viambatanishi vyake vyote vya msingi ikiwemo kofia ngumu na ‘’gloves’’ za kuvaa mikononi wakati wa
kuendesha.
No comments:
Post a Comment