Tuesday 5 June 2018

Wajasiriamali Mkalama wanufaika

PICHA 10 CHINI:  WAWAKILISHI WA VIKUNDI 10 VYA UJASIRIAMALI  WILAYANI MKALAMA WAKIPOKEA HUNDI ZA MIKOPO YA RIBA NAFUU  KUTOKA KWA MKUU WA WILAYA YA MKALAMA MHE. MHANDISI JACKSON MASAKA JIONI YA LEO.















Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka jioni la leo amevikabidhi vikundi 10 vya ujasiriamali hundi zenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 37.8  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mwongozo wa bajeti wa Serikali unayoitaka kila Halmashauri kutoa asilimia 10 ya fedha zake kuviwezesha vikundi vya wanawake na vijana mikopo ya riba nafuu.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwenye vikundi 10, saba vya vijana na vitatu vya wanawake ambapo baada ya kukabidhi hundi hizo Mhe. Masaka alivitaka vikundi hivyo kuhakikisha vinatumia fedha hizo kufanyia shughuli za maendeleo ili viweze kupata faida na kurejesha fedha walizopewa ili watoe fursa ya vikundi vingine kukopeshwa kwa haraka.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhandisi Godfrey Sanga alisema kuwa fedha Halmashauri hiyo itaendelea kutoa fedha zaidi  kwa vikundi kulingana na ongezeko la mapato yake ya ndani.

No comments:

Post a Comment

HALMASHAURI YA WILAYA MKALAMA