Saturday 4 June 2016

KILA ANAYEINGIA NA KUTOKA MKALAMA ACHUNGUZWE-NGUBIAGAI

Mwenyekiti wa kijiji cha Mgolombyo George Nkango akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya aweze kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho.

Kaimu afisa ardhi wa Wilaya ya Mkalama, Imikigwe Mwanitu akitoa ufafanuzi kwa wananchi wa Kijiji cha Mgolombyo  juu ya suala la shamba lao  lililochukuliwa na kijiji cha Kinyambuli.

 PICHA TATU ZINAZOFUATA CHINI  NI SEHEMU YA WANANCHI WA KIJIJI CHA MGOLOMBYO WALIOJITOKEZA KUMSIKILIZA MKUU WA WILAYA YA MKALAMA MHE: CHRISTOPHER NGUBIAGAI NA UJUMBE WAKE.



Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Christopher Ngubiagai akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mgolombyo alipowatembelea jana.

Diwani wa kata ya Miganga Mhe: Omary Mtinga maarufu kama "Kulwa" akimpongeza na kutoa shukrani zake kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkalama mara baada ya kiongozi huyo kumaliza hotuba yake.
Kufuatia kushamiri kwa  matukio ya hivi karibuni ya mauai ya watu kwa kuchinjana, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Christopher Ngubiagai ametoa angalizo kwa wakazi wote wa Mkalama kuwa makini na wageni wote wanaoingia na kutoka Wilayani hapa.

Mhe: Ngubiagai ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama amesema kuwa Vikosi vya Ulinzi na Usalama Wilayani hapa vimejipanga kukabiliana na aina yoyote ya uhalifu lakini vinahitai ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wananchi ili viweze kutimiza majukumu yake ipasavyo.

“Mtu anakuja, anaulizia chumba lakini cha ajabu kila bei unayomtajia hashtuki wala habishi anakuwa tayari kutoa, Jiulize amekuja kufanya nini cha thamani ya pesa anayolipia pango kwa gharama kubwa?” Alisema Ngubiagai.

Ngubiagai aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mgolombyo kilichopo katika kata ya Miganga Wilayani hapa ambapo alitoa wito  kwa watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha wanajiridhisha na kila mtu anayeingia wilayani hapa ikiwa ni pamoja na kufanya utambuzi wa kina juu ya madhumuni ya safari yake.

“Hivi sasa binadamu amekuwa na roho mbaya kuliko hata mnyama kwa sababu wanyama huwa wanaua wanyama wenzao kwa ajili ya kupata kitoweo lakini binadamu anamuua mwenzake tena kwa kumchinja bila kutegemea chochote kutoka kwake”, Aliongeza Ngubiagai.

Kwa upande mwingine, Mhe: Ngubiagai aliwaomba wananchi wa kijiji cha Mgolombyo kuweka akiba ya kutosha ya chakula kutokana na mazao mengi waliyoyapata msimu huu ili kuhakikisha hakuna uhaba wa chakula utakaojitokeza kwa wakazi hao msimu huu.

“Ni aibu kubwa kwa mwananchi ambaye alilima mazao na yakastawi vizuri kisha akayauza na baadaye akaja ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuomba chakula kwa sababu sio tu unajiabisha wewe bali unaniabisha hata mimi kama Mkuu wa Wilaya” Alisema Ngubiagai.

Katika hatua nyingine Mhe: Ngubiagai aliwahakikishia wananchi wa kijiji cha Mgolombyo kuwa atapambana mpaka dakika ya mwisho kuhakikisha kuwa wanapata haki yao ya kurejeshewa shamba lao la kijiji ambalo limeporwa na watu wa kijiji cha Kinyambuli.

“Kwa sasa kesi hii ipo mahakamani hivyo siwezi kuingilia shughuli za mahakama lakini nawahakikishia ntahakikisha haki juu ya suala hili inatendeka kwa sababu mazingira ya uchukuaji wa shamba hili yanazua maswali mengi sana na kwa kuanzia nitaikabidhi Takukuru na Maafisa usalama wa Wilaya majina ya waliokuwa wajumbe wa baraza la ardhi la kata ili kufanya uchunguzi wa kina dhidi ya baraza hilo lililoridhia shamba hilo wapewe watu hao” Alimalizia Ngubiagai.

MSIKILIZE HAPA MHE: NGUBIAGAI AKIZUNGUMZIA SUALA LA ULINZI NA USALAMA WA WILAYA.

1 comment:

HALMASHAURI YA WILAYA MKALAMA