Kilimo cha nyanya Gumanga. |
Kilimo hiki cha
mazao ya bustani kinawafaidisha sana wakazi hawa kwani wanaweza kulima misimu mitatu kwa mwaka na gharama ya kulima ni ndogo. Wastani wa mapato kwa ekeri ni Tshs 8,540,000/=, kila msimu wanaweza kupata faida ya Tshs 4,000,000/= (milioni nne) .Hivyo kwa mwaka huwa
na kipato cha wastani wa Tshs. 12,000,000/=. Kwa ujumla pamoja na shughuli zao za kila siku za kilimo cha mazao mengine kama Uwele, mtama, mihogo, vitunguu
na alizeti, ambayo huwaingizia kipato. Wakazi hawa wana uhakika wa kupata mapato ambayo
hayana tofauti na kima cha chini cha mshahara wa mtumishi wa Serikali.
Wanaishukuru
Serikali ya awamu ya nne na Viongozi wake wote kwa kuwajali wajasiriamali
wadogo Vijijini kwa kuwaboreshea maisha, pia wanaishukuru Halmashauri yao ya Wilaya ya Mkalama kwa kuwawezesha kupata
pembejeo za kilimo na zana za kumwagilia zenye thamani ya tshs 940,000/=ili waweze
kuzalisha kwa njia za kisasa.
No comments:
Post a Comment