Viongozi mbalimbali wa serikali wa serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wameendelea na ziara za kikazi ndani ya wilaya ya Mkalama
ambapo leo ilikuwa ni zamu ya Naibu waziri wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya
jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Daktari Faustine Ndugulile.
Mhe. Ndugulile aliipongeza wilaya ya Mkalama kwa jitihada
za dhati za kuhakikisha wanapanda katika vigezo vya ubora wa utoaji wa huduma
za afya au “Star rating” kama inavyojulikana kitaalam ambapo mwaka 2016
vituo vyote vilikuwa chini ya nyota 3
hali iliyoashiria hakuna kituo kilichokuwa kimekidhi viwango vya utoaji wa
huduma bora.
“Lakini mwaka 2018 asilimia 33.5 ya vituo vilivyopo hapa
Mkalama vimepata nyota 3 au zaidi huku aslimia
66.5 ya vituo vikiwa na nyota 2 na hakuna hata kituo kimoja kisicho na nyota
hivyo jambo lililoifanya Wilaya ya Mkalama kuwa ya tatu kwa mkoa wa Singida kwa
upande wa utoaji wa huduma bora za Afya, hongereni sana” Alisisitiza Mhe.
Ndugulile.
Akiwa katika eneo lililoandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali
ya Wilaya, Mhe. Ndugulile aliwapongeza wananchi wa kata ya Nduguti kwa
kujitolea eneo kwa ajili ya kujenga hospitali ya Wilaya bila fidia yoyote
ambapo aliwataka wananchi wa maeneo mengine nchini kuiga mfano huo.
Mhe. Ndugulile alimalizia ziara yake kwa kutembelea kituo
cha afya cha Kinyambuli ambapo alizipongeza kamati zote zilizoshiriki katika
ujenzi wa kituo hicho na kumuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya
ya Mkalama kuhakikisha anatumia fedha za mapato ya ndani kumalizia kazi zote zilizobaki
za ujenzi wa kituo kufikia mwisho wa mwaka huu ili kuanzia mapema mwakani
wananchi waanze kupatiwa huduma katika majengo hayo mapya.
“Lakini pia niwatangazie wananchi wa Kinyambuli na
Watanzania wote kuwa hivi sasa tumeanza kudhibiti dawa tunazosambaza kwa
kuziwekea alama inayosomeka “MSD GOT” ambayo mbali na kuiweka nje ya maboksi ya
dawa pia tumeiweka mpaka ndani kwenye tembe na kwenye bomba za sindano hivyo
yoyote atakayeona vifaa tiba na dawa zenye alama hiyo zinauzwa kwenye maduka
binafsi ya dawa tafadhali atoe taarifa kwenye mamlaka za Ulinzi na usalama”
Aliongeza Mhe. Ndugulile.
Kwa mwaka 2018 serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
imetumia zaidi ya shilingi bilioni 5.3 kwa ajili ya ukarabati na uwekaji wa
miundombinu ya Afya mkoani Singida ambapo pia imeuongezea Mkoa huo bajeti ya
Afya kutoka shilingi bilioni 4 ya mwaka 2017/2018 hadi shilingi bilioni 7.5 kwa
mwaka 2018/2019.
Jammy's Casino - LONDON, November 23, 2018 - JTM Hub
ReplyDeleteJammy's Casino 여주 출장마사지 - 정읍 출장안마 LONDON, November 23, 2018. £2.2. 제천 출장샵 Add to cart. Add to cart. Category: 충주 출장샵 Casino. Add to cart. Category: Casino. Add to cart. Category: Casino. Add 김천 출장샵 to cart.