MIFUGO NA UVUVI


Idara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza shughuli zake kwa kuzingatia sera ya Uvuvi ya mwaka 2003 na Sera ya mifugo ya mwaka 2006 ambayo inasisitiza ufugaji wa kibiashara wenye tija na ushindani wa kimataifa katika Uvuvi na ufugaji. Kuunga mkono wafugaji wadogo ili waweze kuwa wajasiriamali wazuri. Vilevile kuwa na matumizi endelevu ya rasilimali za Mifugo na Uvuvi ili kuwa na matumizi endelevu ya rasilimali hizo.
Pia pamoja na mambo mengine ina jukumu la kuimarisha huduma za kiuchumi kwa jamii ili iweze kuwa na maisha bora na kufikia malengo ya MKUKUTA, Millenia na hatimaye Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025.

MAWASILIANO:
JINA
NAFASI/CHEO
NAMBA YA SIMU
ELIAS E.MBWAMBO
MKUU WA IDARA
0789111720
0765028840
ABDALAH KHAMIS
AFISA UDHIBITI WA MAGONJWA/ MAJOSHO NA UKAGUZI WA NYAMA
0786347317
ABRAHAM MRINDOKO
AFISA MINADA
0788908933
BENEDICTO MABUBI
AFISA UVUVI
0758506008

2.  TAKWIMU ZA IDARA
S/N
AINA YA WANYAMA
IDADI
1
Ng’ombe
126434
2
Mbuzi
104335
3
Kondoo
47,720
4
Punda
6202
5
Nguruwe
3518
6
Kuku
303402
7
Mbwa
9529

3.   MIUNDOMBINU
S/N
MAJOSHO
VITUO VYA AFYA YA MIFUGO
MINADA
MALAMBO
MABANDA YA NGOZI
MASHAMBA YA MIFUGO
1
21
6
9
15
3
1

Idadi ya Kaya za wafugaji 12,645


4.   MALENGO YA IDARA
Katika kipindi cha 2015/16 hadi 2016/17 Idara inategemea kuendelea kutoa huduma zake ikiwa ni pamoja na Elimu kwa wafugaji,juu ya utengaji wa maeneo ya malisho na kuyaendeleza. uboreshaji koosafu za mifugo pamoja na miundo mbinu ya huduma za mifugo. pia ufugaji wa samaki  Tiba, Kinga kwa mifugo yote pamoja na kuboresha mifugo iliyopo kama ratiba iliyoambatanishwa inavyoonyesha:

RATIBA YA KINGA YA MAGONJWA YA MIFUGO KWA MSIMU WA MWAKA 2016 WILAYA YA MKALAMA.

UGONJWA
JANUARI
FEBRUARI
MARCH
APRIL
MEI
JUNI
JULAI
AGOST
SEPTEMBA
OKTOBA
NOVEMBA
DESEMBA
MDONDO (NEWCASTLE)














KICHAA CHA MBWA (RABIES)














CHAMBAVU NA VIVIMBE VYA NGOZI (BQ & LUMPY SKIN)














UOGESHAJI (DIPPING)














DAWAYA MINYOO (DEWORMING)












MAFUNZO NA MIKUTANO(TRAINNING AND MEETINGS)













5.     MAFANIKO
     i.        Utoaji wa Elimu na kufanya mikutano mbalimbali ambayo imechangia kuleta mahusiano mazuri kati ya Idara na Wananchi na ndiyo siri kubwa iliyowezesha kufanikisha malengo tuliyoyapanga.
    ii.        Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika kuandaa na kutekeleza majukumu ya Idara kumechangia kufanikisha malengo hayo ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu, kutoa dawa za chanjo na kusaidia gharama za uendeshaji wa jumla wa huduma ya kinga ya mifugo ndani ya Wilaya. Wadau hao ni pamoja na Full Dimmension, Arusha Seed Co LTD, Alpha Vety, na TVLA.
  iii.        Idara imefanikiwa kudhibiti magonjwa ya mifugo kwa kutoa chanjo na kuogesha mifugo yote ndani ya Wilaya kiasi cha kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa ya Kideri kwa Kuku, Lumpy skin, Chambavu, na Ndigana Kali(ECF) kwa asilimia 85 (85%)

  iv.        Katika kutekeleza ratiba yetu ya mwaka 2016 imefanyika chanjo ya Mbwa na Kuku kwa awamu ya kwanza kama ifuatavyo
S/N
AINA YA CHANJO
MIFUGO
LENGO
CHANJWA
% YA UTEKELEZAJI
MAELEZO
1
LSD
Ng’ombe
126434
-
0
Uchanjaji haujaanza
2
PPR
Mbuzi
104335
-
0
Uchanjaji haujaanza


Kondoo
47720
-
0
Uchanjaji haujaanza
3
Newcasttle
Kuku
303402
233620
77
-
4
Rabbies
Mbwa
9529
2365
25
Chanjo inaendelea

CHANGAMOTO
·        Mwamko mdogo wa wananchi katika kuchangia ukarabati wa miundo mbinu ya mifugo katika maeneo yao.
·        Uhaba wa vitendea kazi kwa wataalam katika kusimamia na kutekeleza majukumu ya Idara kama vile usafiri.
·        Kutokupewa bajeti tunayoiomba kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za

Idara ikiwemo ununuzi wa madawa mbalimbali na vifaa vya kufanyia kazi.
·        Idara kutopewa 15% ya mapato yatokanayo na mapato ya Mifugo na Uvuvi ambayo husababisha kutokuwepo kwa uendelevu wa sekta hii.
·        Mwamko mdogo wa wafugaji juu ya kukinga Mifugo yao kwa njia ya chanjo na uogeshaji.
·        Serikali za Vijiji kutokuzingatia mgawanyo wa matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya kilimo, ufugaji makazi na huduma mbalimbali za jamii.

UFUMBUZI
1.                 Kuendelea kuhamasisha wananchi kutoa michango kwa ajili ya ukarabati wa miundo mbinu ya mifugo katika maeneo yao.
2.                 Kupatiwa vitendea kazi na madawa ili kufanikisha utoaji wa huduma kwa wafugaji.
3.                 Kutengewa bajeti ya Idara ya Mifugo kama Idara ya kiuchumi tuliyoiomba kwa ajili ya kufanikisha utoaji huduma mbalimbali kwa wafugaji.
4.                 Idara kutengewa na kupewa 15% ya mapato yatokanayo na mapato ya Mifugo/Uvuvi
5.                 Kuendelea na juhudi za makusudi kuelimisha wafugaji juu ya umuhimu wa kukinga Mifugo yao dhidi ya magonjwa hatari ya kuambukiza na kutoa kinga kwa njia ya kuogesha mifugo.
6.                 Serikali za vijiji zinashauriwa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya malisho ya Mifugo ili kuondoa uwezekano wa kuzuka kwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo yao na kuheshimu maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya huduma za Mifugo mfano minada, majosho, mapalio, malambo, vituo vya huduma za Mifugo na maeneo ya vibanio (crush) kwa ajili ya kutolea chanjo ya mifugo.





                                     CHANJO  NA KUOGESHA MIFUGO KAMA ZINAVYOFANYWA NA                                        IDARA HII.

Afisa Mifugo kata ya Mwanga akifungua  dawa aina ya Albadip kwa ajili ya kuiweka kwenye maji yatakayotumika kuogeshea mifugo.

Hapa mtaalamu akimwagia dawa hiyo katika maji yatakayotumika kuogeshea mifugo.

Huu ndio muonekano wa maji ya kuogeshea mifugo baada ya kumwagiwa dawa aina ya Albadip.

Mifugo aina ya Ng'ombe na Mbuzi katika kata ya Mwanga ikisubiri kuogeshwa. 

Hivi ndivyo zoezi la kuingiza mifugo katika josho ilivyokuwa ikifanyika.
                                PICHA TATU CHINI ZIKIONESHA NAMNA NG'OMBE                                                              WALIVYOKUWA WAKIOGESHWA.





                                PICHA NNE CHINI ZIKIMUONESHA MTAALAMU WA MIFUGO H/W                                 MKALAMA, JOSEPH MICHAEL AKITOA HUDUMA YA CHANJO                                           KATIKA KATA YA ILUNDA.




Idara ya Mifugo na uvuvi imefanikiwa kuingiza mapato ya kiasi cha shilingi 31,871,500 mpaka sasa kutokana na chanjo ya Ng’ombe, Mbuzi na Kondoo inayoendelea hivi sasa.

Zoezi hilo lipo kisheria chini ya Sheria ya Udhibiti wa Magonjwa ya Mifugo namba 17  ya mwaka 2003 kifungu cha 28 na 62 ambayo inamtaka mfugaji yoyote kuipa kinga mifugo yake na yoyote atakayevunja sheria hiyo adhabu yake ni faini isiyopungua shilingi laki tatu au kifungo cha miezi sita gerezani au adhabu zote kwa pamoja.

Udhibiti wa magonjwa ya mifugo Mkalama hufanyika kila mwaka kwa njia mbili kuu kwa kuzingatia ratiba ya Wilaya ambazo ni Chanjo (Ng'ombe, Mbuzi, kondoo, Mbwa na Kuku) na Uogeshaji mifugo ambayo hufanyika kwa kuogesha mifugo kwenye majosho yaliyopo ndani ya Wilaya ili kudhibiti magonjwa mbalimbai yaenezwayo na Kupe kama vile Ndigana Kali (ECF), Ndigana baridi (Anaplasmosis), Mkojo damu (Babesiosis) na  Majimoyo (Heart water).

Hii pia huambatana na udhibiti wa visumbufu vingine kama vile viroboto, Ndorobo na Chawa.

Njia ya pili ni udhibiti wa vidusi vya ndani (Internal Parasite) kama vile minyoo aina zote kwa njia ya chanjo (vaccination) au kunywesha dawa za minyoo (deworming).

Katika zoezi hilo, Ng’ombe wanapewa chanjo ya dawa aina ya Lumpy Skin ambayo husaidia kuondoa na kukomesha maradhi mbalimbali yanayosumbua mifugo hiyo.

Kwa upande wa mbuzi, dawa aina ya Ivomectin ndio iliyotumika katika chanjo hiyo ambayo ina nguvu na uwezo maradufu ya dawa nyingine katika kukinga maradhi ya mifugo hiyo.

Idara ya Mifugo na uvuvi inapenda kutoa rai kwa wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha mifugo yao imepatiwa chanjo ili kuepukana na magonjwa mbalimbali ambayo yamekuwa yakigharimu vifo vingi vya mifugo.

Aidha Idara ya Mifugo na Uvuvi imeanzisha zoezi la uogeshaji wa mifugo katika kata zote ambapo zoezi hilo limeanzia kwenye kata ya Mwanga.

Baada ya dawa nyingine kuonekana kutosaidia kuondoa kabisa wadudu katika mifugo hiyo wakati wa zoezi la kuogesha , idara imeamua kutumia dawa aina ya Albadip ambayo imeonekana kumaliza kabisa tatizo la wadudu wanaosumbua mifugo hiyo.

IFUATAYO NDIO RATIBA YA UDHIBITI WA MAGONJWA YA KIFUGO KATIKA WILAYA YA MKALAMA KWA MWAKA 2016/2017.



1 comment:

  1. Mhhhhh... Some amazing work my boy... Keep up the good work.

    ReplyDelete

HALMASHAURI YA WILAYA MKALAMA